Wamarekani watapiga kura mwezi Novemba kumchagua rais ajaye wa Marekani. Kura hiyo itafuatiliwa kwa karibu kote ulimwenguni.
Pia watakuwa wakipigia kura wabunge wa Baraza la Congress, ambao wanachukua sehemu muhimu katika kupitisha sheria ambazo zinaweza kuwa na athari kubwa kwa maisha ya Marekani.
Uchaguzi ujao wa rais wa Marekani ni lini?
Uchaguzi wa 2024 utakuwa Jumanne, tarehe 5 Novemba 2024. Mshindi atahudumu kwa muda wa miaka minne katika Ikulu ya White House, kuanzia Januari 2025.
Rais ana uwezo wa kupitisha baadhi ya sheria peke yake lakini zaidi lazima ashirikiane na Congress kupitisha sheria.
Katika hatua ya dunia, kiongozi wa Marekani ana uhuru mkubwa wa kuwakilisha nchi nje ya nchi na kubuni sera za kigeni.
Kocha wa zamani wa mpira wa miguu na mwalimu - sasa ndiye mgombea mwenza wa Harris
'Je, ni Mwafrika au Mhindi?': Trump ahoji utambulisho wa rangi wa Harris
See AlsoLe futur Tesla Model Y sera-t-il disponible en 6 ou 7 places ?Bilan démographique 2023 de l’Île-de-France : des naissances toujours en baisse - Insee Flash Ile-de-FranceRégion Île-de-France : départements, carte, localisation et logo.US Open 2024 live updates: Taylor Fritz, Jannik Sinner advance to final with tough yet different wins
Wagombea ni akina nani na wanateuliwa vipi?
Vyama viwili vikuu huteua mgombea urais kwa kupigia kura msururu wa kura zinazoitwa chaguzi za mchujo za majimbo na vikao, ambapo watu huchagua wanayemtaka kukisimamia chama katika uchaguzi mkuu.
Katika Chama cha Republican, Rais wa zamani Donald Trump alipata uungwaji mkono wa chama chake kwa kupata uungwaji mkono mkubwa dhidi ya wapinzani wake. Akawa mteule rasmi wa Republican katika kongamano la chama huko Milwaukee, Wisconsin.
Kwa Democrats, Makamu wa Rais Kamala Harris anakaribia uteuzi. Alijiunga na kinyang'anyiro hicho baada ya Rais Joe Biden kujiondoa.
Bi Harris anaonekana kuwa na uungwaji mkono usiopingika ndani ya chama chake na anaweza kuidhinishwa katika kongamano lake mwezi Agosti, huko Chicago.
Pia kuna baadhi ya wagombea binafsi wanaowania urais, akiwemo Robert F Kennedy Jr, mpwa wa rais wa zamani John F Kennedy.
Je, Democrats na Republicans wanasimamia nini?
Democrats ni chama cha huria cha kisiasa, chenye ajenda iliyofafanuliwa kwa kiasi kikubwa na msukumo wake wa haki za kiraia, usalama wa kijamii na hatua za kushughulikia mabadiliko ya hali ya tabia nchi.
Republican ni chama cha kisiasa cha kihafidhina nchini Marekani. Pia kinajulikana kama GOP, au Grand Old Party, kimetetea kodi ya chini, kupunguza ukubwa wa serikali, haki za bunduki na vikwazo vikali zaidi kwa uhamiaji na utoaji mimba.
Je, uchaguzi wa rais wa Marekani unafafanyika vipi?
Mshindi sio mtu ambaye anapata kura nyingi kote nchini.
Badala yake, wagombea wote wawili hushindana ili kushinda mashindano yanayofanyika katika majimbo 50.
Kila jimbo lina idadi fulani ya kinachojulikana kama kura za chuo cha uchaguzi kulingana na idadi ya watu. Kuna jumla ya kura 538 , na mshindi ni mgombea ambaye atashinda 270 au zaidi.
Majimbo yote isipokuwa mawili yana kanuni ya mshindi-wote, kwa hivyo mgombea yeyote atayeshinda idadi kubwa zaidi ya kura hutunukiwa kura zote za chuo cha uchaguzi cha jimbo.
Majimbo mengi yanaegemea sana upande mmoja au mwingine, kwa hivyo mwelekeo huwa katika majimbo kadhaa au hivyo lengo huwa ni kupata ushindi katika majimbo kama 12 . Haya hujulikana z kama uwanja wa vita au swing states [Majimbo yenye kura zisizotabirika]
Inawezekana kwa mgombea kushinda kura nyingi zaidi kitaifa - kama Hillary Clinton alivyofanya mwaka wa 2016 - lakini bado ashindwe katika chuo cha uchaguzi.
Nani mwingine anachaguliwa?
Macho yote yatakuwa ni kwa nani atakayeshinda urais, lakini wapiga kura pia watakuwa wakichagua wanachama wapya wa Congress - ambako sheria zinapitishwa – watakapokuwa wakijaza karatasi za kura.
Bunge la Congress linajumuisha Baraza la Wawakilishi, huku viti vyote 435 vikitarajiwa kukupigiwa kura, na Seneti, ambapo viti 34 vinagombaniwa.
Warepublican kwa sasa wanadhibiti Ikulu, ambayo huanzisha mipango ya matumizi. Wanademocrat wanasimamia Seneti, ambayo hupigia kura uteuzi muhimu serikalini.
Mabunge haya mawili yanapitisha sheria na yanaweza kuwa kama ukaguzi wa mipango ya Ikulu ya Marekani iwapo chama tawala katika bungee lolote halikubaliani na rais.
Ni lini tutajua nani ameshinda uchaguzi?
Kawaida mshindi hutangazwa usiku wa uchaguzi, lakini mnamo 2020 ilichukua siku chache kuhesabu kura zote.
Kipindi cha baada ya uchaguzi kinajulikana kama mpito ikiwa kuna mabadiliko ya rais.
Ni wakati wa utawala mpya, ikiwa ni pamoja na mawaziri, kuunda na kupanga mipango ya muhula mpya.
Rais anaapishwa rasmi kushika wadhifa huo mwezi Januari katika hafla inayojulikana kama kuapishwa, inayofanyika kwenye ngazi za jengo la Capitol - Washington DC.
Nani anaweza kupiga kura?
Ikiwa wewe ni raia wa Marekani na una umri wa miaka 18 au zaidi, unapaswa kuwa umetimiza masharti ya kupiga kura katika uchaguzi wa urais, ambao hufanyika kila baada ya miaka minne.
Wajue wagombea wa urais Marekani waliogombea wakiwa gerezani
Marais wa Marekani waliouawa na walionusurika kuuawa wakiwa wagombea
Imetafsiriwa na Dinah Gahamanyi